Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania

TanTrade Fostering Business

TANTRADE NA WRRB KUTOA MAFUNZO YA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA

  • August 29, 2023

..........................
Na. Norah Thomas-TanTrade 
Dar es salaam.
28 Agosti 2023.


Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) kwa kushirikiana na BODI ya usimamizi wa stakabadhi za  ghala (WRRB) Tarehe 28 Agosti 2023  watoa Mafunzo ya utekelezaji  wa mfumo wa stakabadhi za ghala   yenye  lengo la kuwajenga uwezo  Watendaji  wa Kampuni za waendesha ghala,  Wasimamizi wa Ghala,  Meneja Dhamana  pamoja na washiriki binafsi, Mafunzo yatadumu kwa muda wa siku 5 kuanzia Tarehe 28 Agosti mpaka Tarehe 1 septemba 2023.

Akizungumza katika Mafunzo hayo,  Mkuu wa  wilaya ya Ubungo, Hashim Komba  katika ukumbi wa Kilimanjaro uliopo katika Uwanja wa  Maonesho ya Sabasaba,alisema  mafunzo hayo yanakwenda kuongeza heshima kwa watendaji wa ghala na kupelekea utoaji wa huduma bora kwa  Wadau wote.

Amesema bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala inatakiwa  kuongeza matumizi ya TEHAMA katika utendaji ili kuendana na mabadiliko ya dunia.

Naye Mkurugenzi wa huduma za uendeshaji  wa Biashara kutoka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) Bi. Mary Fidelis amesema kuwa  TanTrade ipo tayari kutoa ushirikiano wa kiutendaji   ili  kuwajengea uwezo  Watendaji  wa Kampuni za waendesha ghala,  Wasimamizi wa Ghala,  Meneja Dhamana  pamoja na washiriki binafsi.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa  Stakabadhi  za Ghala  Asangye Bangu amesema kuwa  lengo kubwa la mafunzo hayo ni  kuongeza tija katika ufanyaji  kazi na matarajio ya mafunzo  hayo ni kuhakikisha kazi zinafanywa  kwa usahihi kwa kuzingatia sheria .

Bangu  ameongeza kuwa Bodi ya Udhibiti na Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala imejipanga kuona ambavyo watendaji hao  watatekeleza shughuli zao za kiserikali kwani wamejitaidi kuingiza bidhaa mbalimbali kadiri sheria ilivyo waruhusu kufanya  hivyo.

‘’nilipofanya ukaguzi nilibaini changamoto mbalimbali  kwenye maghala, anaeshikiliwa kwanza ni Meneja na Mkurugenzi anakuwa hayupo ukimuuliza  Mkurugenzi anakuambia Meneja wangu ndio anaehusika, kwahiyo mda mwingine unakuta meneja hana Taharifa, hivyo natoa wito kwa Washiriki wote kuzingatia Mafunzo yanayotolewa ili kuwaongezea uwezo wa Kiutendaji. Alisema