Kikao cha Kimkakati Kati ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania na Idara ya Uhamiaji
- April 17, 2026
Kikao cha Kimkakati
kati ya TanTrade na Idara ya Uhamiaji
Tarehe 16 April
2026, Dar es Salaam
Mamlaka ya Maendeleo
ya Biashara Tanzania (TanTrade) imefanya kikao cha kimkakati na Idara ya
Uhamiaji kwa lengo la kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma na kuimarisha
mazingira ya biashara nchini.
Mazungumzo haya yamejikita katika maeneo muhimu
yafuatayo:
a)
Uratibu
wa misafara ya kibiashara ndani na nje ya nchi ili kurahisisha safari za wafanyabiashara na
wawekezaji, huku taratibu za uhamiaji zikiboreshwa kwa ufanisi na usalama.
b)
Kuimarisha
makongamano na mikutano ya kimataifa kwa kuhakikisha usalama wa wageni wa kimataifa na Watanzania
wanaoshiriki katika majukwaa ya nje ya nchi, ili kulinda maslahi ya taifa na
kuimarisha diplomasia ya kiuchumi.
c)
Kuboresha
maandalizi ya maonesho ya biashara ya kimataifa na dunia (EXPOs) yanayofanyika Tanzania na nje ya mipaka, kwa
kuweka mifumo thabiti ya usalama na huduma bora kwa washiriki.
d)
Kujenga
mazingira rafiki ya biashara
kwa kushirikisha taasisi muhimu katika kukuza shughuli za kibiashara na
uwekezaji, na kuhakikisha Tanzania inakuwa kitovu cha mikutano na maonesho
yenye tija na manufaa kwa uchumi wa taifa.
Kikao hiki kimeweka
msingi wa ushirikiano wa karibu kati ya TanTrade na Idara ya Uhamiaji, ambacho
kitasaidia:
a)
Kuimarisha
usalama wa Watanzania wanaoshiriki mikutano na makongamano nje ya nchi,
kwa kuhakikisha wanapata ulinzi wa kisheria na kiutawala wanapokuwa katika
majukwaa ya kimataifa.
b)
Kuongeza mapato
ya taifa kupitia sekta ya biashara, utalii wa mikutano (MICE), na uwekezaji
wa moja kwa moja wa kigeni.
c)
Kuweka
Tanzania katika nafasi ya kipekee kama kituo ya kimataifa ya biashara na
uwekezaji, yenye usalama, tija na manufaa kwa uchumi wa taifa.
Kikao cha kimkakati
kati ya TanTrade na Idara ya Uhamiaji kimeweka msingi wa ushirikiano thabiti
unaolenga kurahisisha safari za kibiashara, kuimarisha maandalizi ya maonesho
na mikutano ya kimataifa, na kujenga mazingira rafiki ya uwekezaji, huku kikipa
kipaumbele kwa usalama wa wageni wanaokuja Tanzania na Watanzania wanaoshiriki
mikutano nje ya nchi, hatua inayojenga taswira ya taifa kama kitovu cha
biashara na uwekezaji barani Afrika.