KAMATI YA MAANDALIZI YA MAONESHO SABASABA 2026 YAKUTANA
- April 2, 2026
Dar es Salaam, 01
Aprili 2026
Kamati ya Maandalizi
ya Maonesho ya Sabasaba 2026 imekutana katika makao makuu ya TanTrade kujadili
mikakati ya kuboresha mchakato wa maandalizi ya maadhimisho ya miaka 50 ya
SABASABA 2026.
Katika kikao hicho,
Mkurugenzi wa TanTrade, Dkt. Latifa Khamis, aliwasilisha mkakati wa awali wa
maandalizi, ukilenga kuhakikisha maonesho ya mwaka 2026 yanatekelezwa kwa
viwango vya juu vya ubora na kuvutia washiriki wengi zaidi kutoka ndani na nje
ya nchi.
Baada ya mawasilisho
hayo, Mwenyekiti wa kikao, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara,
Bw. Aristides Robert Mbwasi, aliridhishwa na hatua zilizofikiwa katika
maandalizi ya maonesho. Aidha, alisisitiza umuhimu wa kuongeza kasi ya
utekelezaji kwa kuwa maonesho haya ni ya kihistoria na yana nafasi kubwa katika
kuchochea maendeleo ya biashara na uchumi wa taifa.
Vilevile, wajumbe wa
kamati walijadili masuala ya ushirikishwaji wa wadau mbalimbali, ikiwemo sekta
binafsi, mashirika ya kimataifa, na washirika wa maendeleo, ili kuhakikisha
maonesho ya mwaka huu yanakuwa jukwaa la kimataifa la biashara na uwekezaji. Pia
walisisitiza umuhimu wa kuimarisha kampeni za uhamasishaji ndani na nje ya
nchi, hususan kupitia vyombo vya habari na majukwaa ya kidigitali, ili kuongeza
idadi ya washiriki na wageni wa kimataifa.
Kamati ilikubaliana
pia kuimarisha maandalizi ya maonesho kwa kuzingatia vipengele vya ubunifu,
teknolojia, na urithi wa kitamaduni wa Tanzania, ili kuonyesha sura halisi ya
maendeleo ya viwanda na biashara kwa kipindi cha nusu karne.
Kwa pamoja, wajumbe
walitoa wito wa mshikamano na mshirikiano wa kitaifa katika kuhakikisha
maonesho ya SABASABA 2026 yanakuwa ya kipekee, yenye tija, na yanayoacha alama
ya kudumu katika historia ya taifa.