RASIMU ZA KANUNI MPYA ZA BIASHARA 2026 ZAWASILISHWA KWA WADAU
- March 11, 2026
Dar es Salaam; 11 March 2026
_____________________________________________
Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara
Tanzania (TANTRADE) imewasilisha rasimu za kanuni mpya za biashara kwa mwaka
2026 kwa wadau, zikiwa na lengo la kuongeza ushindani wa bidhaa na Tanzania
katika masoko ya ndani na ya kimataifa. Kanuni hizi zinahusu maeneo muhimu kama
vile mauzo ya nje, masoko mapya, maonesho ya biashara, taarifa za masoko,
kuendeleza wafanyabiashara wadogo na wa kati, pamoja na utangazaji wa bidhaa kupitia
nembo ya “Made in Tanzania.”
Rasimu zilizopendekezwa
zinajumuisha kanuni za kuratibu ushirikiano wa taasisi za Serikali na sekta
binafsi, kanuni za tozo, matumizi ya alama ya rajamu ya Taifa, na kanuni za
ukuzaji wa maonyesho ya biashara ili kuimarisha uwazi, utawala bora na
ushindani wa bidhaa za Tanzania.
TANTRADE inahimiza wadau wa sekta
ya biashara, uzalishaji, uwekezaji na usafirishaji kusoma rasimu hizi na
kuwasilisha maoni yao kwa maslahi ya Taifa. Ushirikiano wa wadau ni msingi wa
mafanikio ya mchakato huu, kwani unahakikisha kanuni zinakuwa shirikishi na
zenye tija kwa manufaa ya nchi.