Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania

TanTrade Fostering Business

Ufunguzi rasmi wa Maonesho ya Sita ya Bidhaa na Huduma (6th International Import Expo - CIIE ) ya Shanghai - China ambayo yameanza tarehe 5 hadi 10 Novemba, 2023

  • November 7, 2023

Maonesho hayo ambayo yanatoa fursa kwa nchi mbalimbali kuuza bidhaa nchini China yalifunguliwa rasmi na Waziri Mkuu wa China  Mheshimiwa Li Qiang.

Katika Maonesho haya nchi zaidi ya 127 zinashiriki zenye zaidi ya Waoneshaji 2800. Aidhaa bidhaa mbalimbali za Kilimo, Mazao Teknolojia na Ubunifu mpya 438 zenye thamani ya dola za Kimarekani bilioni 73.52 zinaoneshwa.

Katika Maonesho haya kutakuwa na mikutano 24 ya kibiashara na uwekezaji ambayo itahudhuriwa na Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, Taasisi za Biashara na Uwekezaji na Sekta Binafsi wakikutanishwa na taasisi mbalimbali na wawakilishi wa jumuiya za kimataifa wakiwemo ITC, WTO UNDP na UNIDO.

Aidha, katika mikutano hiyo fursa mbalimbali za kibiashara na uwekezaji zitajadiliwa kwa undani.

Maonesho haya ya 6 ya Huduma na Bidhaa ya China (CIIE) ni fursa nzuri kwa wafanyabiashara watanzania kuonesha Bidhaa na Huduma zao kwa jamii ya China na kuweza kuwaunganisha na masoko ili kukuza mitaji yao na kukuza uchumi wa Taifa kiujumla.

Msafara wa washiriki kutoka Tanzania katika Maonesho haya waliongozwa na Maafisa kutoka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) chini ya Mkurugenzi wa Ukuzaji Biashara, Bw. Fortunatus Mhambe. Washiriki katika Maonesho haya kutoka Tanzania ni pamoja na ZAFICO, PBZ, TRA, ZBS, Africafe na KMVL.

Aidha, TANTRADE imesimamia ushiriki wa baadhi ya makampuni na taasisi  ambazo zimewasilishwa sampo bila ushiriki wao binafsi ikiwamo kampuni Ya AMIMZA inayouza kahawa nje ya nchi.