Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania

TanTrade Fostering Business

Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano, TANTRADE wakutana na East Africa Commercial and Logistics Center (EACLC)- Shanghai

  • November 7, 2023

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini China, Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Nyumba Zanzibar Dkt. Mngereza Mzee Miraji wawakilishi wa TanTrade wakiongozwa na Mkurugenzi wa Ukuzaji Biashara Bw. Fortunatus Mhambe na mwakilishi  kutoka Kampuni ya Kahawa ya Africafe Bw. Abdulhakim Mulla walikutana katika ofisi kuu ya EACLC iliyopo Shanghai-China kwa ajili ya kusikiliza wasilisho kutoka kwa Lisa Wang  ambaye ni Mwenyekiti wa EACLC ambaye katika wasilisho lake alishukuru Serikali ya Tanzania kuendelea kuipa fursa ya kiuwekezaji kampuni yake ya EACLC.

Lisa alitumia wasaa huo kuorodhesha miradi ambayo kampuni yake  inaendelea na utekelezaji wake ikiwa ni pamoja na
- Mradi Mkubwa wa Soko Kuu La Kimataifa la Afrika Mashariki -Ubungo Dar Es Salaam linaloendelea na ujenzi wake ambao unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2024 ambao utakuwa na maduka zaidi ya 2,000 na kufanya Jiji la Dar Es Salaam kupokea wageni kutoka takribani nchi 9 ambazo zitakuwa zikinunua bidhaa hapo badala ya kusafiri mpaka nchini China.

-  Mradi wa Ujenzi wa Hospitali Zanzibar na
- Mradi wa Maghala ya Uhifadhi wa Bidhaa  zitakazouzwa nje ya nchi na zitakazoletwa nchini Tanzania utaokuwa maeneo ya Uwanja wa Ndege wa Zanzibar

Vilevile Lisa Wang aliongeza kwa kuishukuru TanTrade kwa kuendelea kuiunga mkono kampuni ya  EACLC na kusema kuwa kutokana na ushiriki wao mzuri katika Maonesho ya Sabasaba {DITF} ya 47 ya 2023 wafanyabiasha wengi zaidi kutoka China wameonesha nia ya kushiriki katika Maonesho yajayo ya 48 ya DITF, 2024.

Aidha, Bi. Lisa Wang ameahidi kuendelea kuitangaza Tanzania ikiwamo kushiriki katika Maonesho yatakayofanyika Januari, 2024 Zanzibar.

Kwa upande wake Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini China alimwakikishia Lisa Wang kuwa Serikali inatambua Mchango Mkubwa EACLC inafanya kwa nchi ya Tanzania na kuwa wataendelea kumpa ushirikiano.

Naye Bw. Fortunatus Mhambe ambaye ni Mkurugenzi wa Ukuzaji Biashara alimpongeza Lisa kwa kuleta washiriki wa Maonesho ya Sabasaba kutoka China wapatao 187. Aidha, alimpongeza Lisa kwa kampuni yake kudhamini Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar Es Salaam ya 2023