Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania

TanTrade Fostering Business

SERIKALI YAENDELEA KUBORESHA HUDUMA ZA TEHAMA NCHINI.

  • July 25, 2023

………………….
Na. Norah Thomas-TanTrade Dar es salaam.
Dar es salaam
8 Julai, 2023.


 Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye   tarehe 8 Julai, 2023  ameyasema hayo,  wakati akifungua rasmi siku maalum ya TEHAMA iliyofanyika  katika Uwanja wa Maonesho wa Mwl. JK Nyerere barabara ya Kilwa Dar es salaam. Mhe. Nape, amewataka Wananchi kuendelea kutumia kila fursa ya TEHAMA sambamba na kuunga mkono juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali katika kuboresha huduma za TEHAMA, lengo hasa ikiwa ni kuifanya Tanzania kuwa na uchumi wa Kidijitali.

Aidha Mhe. Nape akiwa ameambatana na  Naibu waziri Wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Kundo Methew (Mb), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Selestine Gervas Kakele pamoja na Mkurugenzi wa Utawala na Usimazi wa Rasilimaliwatu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bi. Salome Kessy ameeleza mikakati mbalimbali inayoendelea kufanywa na Serikali ya Tanzania katika kufanikisha Tanzania kuwa na Uchumi wa kidijitali.


Pia ameipongeza TanTrade kwa kuonyesha juhudi za kumsapoti Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hasan na  kufanya mapinduzi ya kuboresha Maonesho na kuwafanya Wafanyabiashara pamoja na Watembeleaji kufurahia Maonesho haya ya 47, na kuhaidi Wizara yake  itashirikiana na  TanTrade katika kuboresha miundo mbinu ya TEHAMA kwa Maonesho yajayo.


‘’Baada ya Maonesho haya ya mwaka huu, Katibu Mkuu na Taasisi zetu za Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia  tutakaa na  TanTrade ili  tufanye tathmini ya pamoja  tuone yale maeneo ambayo tunaweza kuboresha  miundo mbinu ya TEHAMA na kuyafanya maonesho yajayo yawe bora zaidi’’.Alisema.


Pamoja na maazimisho ya siku hiyo, Mhe. Nape   amezindua huduma ya Intaneti ya Wazi (Free-Wifi) katika maeneo 17 ndani ya Uwanja wa Maonesho ya Sabasaba), Huduma hiyo ya wazi imewezeshwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kwa kushirikiana na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL).

Vilevile, Mhe. Waziri Nape ametumia nafasi hiyo kuishukuru Serikali ya awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuweka mazingira wezeshi kwa Wizara hii yenye lengo la kurahisisha huduma za TEHAMA nchini.

Naye  Mkurugenzi Mkuu  wa TanTrade Bi. Latifa M. Khamis  ameishukuru Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kupitia mtandao wa TTCL kwa kutoa huduma ya Intaneti ya wazi (Free wifi) katika Maonesho hayo kwani huduma hiyo  imelenga kurahisisha Mawasiliano na kuboresha Maonesho  yawe na mvuto zaidi na kuwasaidia Washiriki pamoja na Watembeleaji kuweza kupata Mawasiliano kwa njia rahisi na kwa haraka zaidi  katika kipindi chote cha Maonesho, pia ameelezea namna ambavyo TanTrade inafanya kazi zake kulingana na mabadiliko ya Teknnolojia kwa kuzindua mifumo mipya mbalimbali ya kigitali ambayo imetumika katika Maonesho ya 47.

‘’ Teknolojia ni kipaumbele katika utendaji wetu wa kazi Hatupo nyuma katika Mabadiliko ya teknolojia ili kurahisisha shughuli za ufanyaji wa  Biashara nchini tumetumia  mifumo mipya mbali ambayo ni pamoja na  mfumo wa kidigitali wa  ugawaji wa nafasi za mabanda , mfumo wa kidigitali wa ugawaji wa  vitambulisho pamoja na mfumo wa kugawa tiketi za kuingia katika Uwanja wa Maonesho.’’ Alisema.

Pia Bi. Latifa aliwapongeza Waandishi wa habari kwa kusapoti na kuyatangaza Maonesho ndani na nje ya nchi.