Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania

TanTrade Fostering Business

WATANZANIA WAALIKWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI KATIKA JIMBO LA HARYANA NCHINI INDIA

  • July 25, 2023


………………….
Na. Norah Thomas-TanTrade Dar es salaam.
Dar es salaam
10  Julai, 2023.

Hayo yameyasemwa  leo tarehe 10 Julai, 2023 na Katibu Mkuu wa Serikali katika jimbo la Haryana Dkt. Raja Sekhar Vundru  Katika Uzinduzi wa siku Maalumu ya Haryana katika Maonesho ya sabasaba, inayofanyika  katika Uwanja wa Maonesho wa Mwl. JK Nyerere barabara ya Kilwa Dar es salaam yenye lengo la kuonyesha fursa za Biashara na Uwekezaji zinazopatikana nchini India katika Jimbo la Haryana pamoja na fursa zinazopatikana nchini Tanzania.

Akizungumza katika Maazimisho ya siku hiyo Dkt. Raja amesema,  Jimbo la Haryana  limejipanga kufanya Biashara na kuwekeza nchini  Tanzania hususani katika  sekta ya elimu, Mashine, kilimo, Afya pamoja  na Sekta ya Matunda,   Pia wanataka kutangaza huduma za TEHAMA, madini na kilimo katika nchi za Afrika, ameongeza kuwa Matunda aina ya Parachichi kutoka  Tanzania yana soko  sana  nchini India, hivyo amewaasa Watanzania kuchangamkia fursa hiyo.

‘’Natoa rai kwa Watanzania kutumia fursa zinazopatikana nchini India katika jimbo la Haryana hususani katika biashara ya Parachichi na matunda mengine kwani Parachichi kutoka Tanzania huwa hazitozwi kodi  hivyo tutumie fursa hiyo ili kuzisogeza nchi zetu mbele’’ alisema.

Pia aliongeza kuwa Serikali ya  India inatoa Mualiko kwa Wafanyabiashara wa Tanzania kwenda kufanya Biashara na  kujionea fursa nyingi zinazopatiana katika jimbo la Haryana,   kwani kuna fursa nyingi za biashara na wametengeneza mazingira mazuri  kwa ajili ya biashara na uwekezaji pia  wanajenga madaraja ya mahusinao kati ya jimbo la  haryana na nchi nyingine ili kusaidia nchi za nje kutumia fursa kujenga mahusiano yatakayokuwa endelevu.
        
Aidha  Mwenyekiti wa Bodi ya Tantrade Profesa  Ulingeta O. Mbamba aliongeza kuwa  katika kuadhimisha siku ya India katika Maonesho 47 ya DITF, tumetambua na kuona umuhimu wa nchi hii kwani India ni nchi ya tatu  (3)  kwa kufanya biashara na Tanzania, na thamani ya biashara kati ya Tanzania na India imefikia kiwango cha dola bilioni 4.58 katika kipindi cha mwaka 2021 mpaka 2022.

 ‘’ Pamoja na kuwa India ni miongoni mwa nchi tunayofanya nayo biashara kwa miaka mingi, pia India ndio nchi yenye  jamii kubwa ya Wageni wanaoishi nchini hivyo  Serikali ya Tanzania kupitia TanTrade itahakikisha  inadumisha Mahusiano mazuri ya kibiashara yaliyopo baina ya Tanzania na India,  pia TanTrade itasimamia  kwa vitendo  Mikataba  ya biashara  na India.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania Bi. Latifa Khamis amesema anaishukuru  sana Serikali ya India kwa kudumisha Mahusiano mazuri na Tanzania, na kwa kupitia Mahusiano hayo yamesaidia kuwepo  Makampuni zaidi ya 50 kutoka jimbo la Haryna ili kuonesha fursa zilizopo katika jimbo la hilo ambalo  linaongoza katika uchumi wa India.

‘’ Msafara  huu umekuja na Makampuni zaidi ya hamsini (50) na viongozi kutoka katika Serikali ya India  jimbo la Haryana waliohudhulia katika  Maonesho  haya ya 47 ya biashara ya Kimataifa  ya Dar es salaam (DITF 2023), kuleta bidhaa zao mbalimbali kwa ajili ya kuonesha na kupata wadau wa kufanya nao Biashara, pia kupitia Maonesho haya tumepata mafanikio ya kutia saini Mikataba mikubwa baina ya Serikali zote mbili hivyo natoa wito kwa Watanzania kujitokeza kwa wingi kuja kujifunza Teknolojia mpya ya uzalishaji wa bidhaa kutoka kwa wageni wetu mbalimbali’’ alisema.