TANTRADE KUSHIRIKI KATIKA UFUNGUZI WA MAFUNZO YA UJASILIAMALI KWA WANAWAKE
- September 12, 2023

DAR ES SALAAM.
12 SEPTEMBA, 2023
Mamlaka ya Maendeleo na Biashara Tanzania (TanTrade) kushiriki na wafanyabiashara katika ufunguzi wa mafunzo na kufanya mdahalo kuhusu Ujasiliamali katika ukumbi wa Kibada Garden Kigamboni- Dar es salaam tarehe 12 Septemba, 2023.
Ambapo, Afisa wa TanTrade Bi.Lulu Masanje amesema Mamlaka ya Maendeleo na Biashara Tanzania inatoa mafunzo juu ya kujikwamua kibiashara ndani na nje ya nchi ambapo jukumu la kwanza ni kutoa taarifa mbalimbali za biashara ambazo zinampa fursa mfanyabiashara kufahamu kuhusu takwimu ambazo bidhaa zinauzwa sana na kuongeza soko kwa wingi zaidi na itamsaidia mfanyabiashara kufanya maamuzi sahihi kwaajili ya kujikwamua kiuchumi.
Vilevile, TanTrade inatoa fursa za masoko, mabanda ya maonyesho na usafirishaji wa bidhaa kwenda nchi mbalimbali ambapo fursa hizi zitachangia katika kuongeza uchumi binafsi na nchi kwa ujumla. Kadhalika, kutambua takwimu za bidhaa zinazouzwa na nchi mbalimbali kama vile korosho, kahawa, pamba na parachichi.
Pia, kuhusu suala la nishati, TanTrade imeweza kushirikiana na Kenya katika usambazaji wa nishati ya kisasa na iliyo salama na itaendelea kujumuisha nchi mbalimbali ilikukuza soko la nishati vilevile,katika mdahalo amewashauri wajasiliamali kuhusu ufanyaji wa utafiti kabla ya kuleta bidhaa sokoni kwani itasaidia katika kutambua mahitaji ya wateja na kupata njia mbalimbali za kuwa hudumia.
Hivyo, TanTrade ina mchango mkubwa kwa wafanyabiashara na itaendelea kushirikiana nao katika kutangaza bidhaa zao ili kukuza soko binfasi na nchi kwa ujumla
12 SEPTEMBA, 2023
Mamlaka ya Maendeleo na Biashara Tanzania (TanTrade) kushiriki na wafanyabiashara katika ufunguzi wa mafunzo na kufanya mdahalo kuhusu Ujasiliamali katika ukumbi wa Kibada Garden Kigamboni- Dar es salaam tarehe 12 Septemba, 2023.
Ambapo, Afisa wa TanTrade Bi.Lulu Masanje amesema Mamlaka ya Maendeleo na Biashara Tanzania inatoa mafunzo juu ya kujikwamua kibiashara ndani na nje ya nchi ambapo jukumu la kwanza ni kutoa taarifa mbalimbali za biashara ambazo zinampa fursa mfanyabiashara kufahamu kuhusu takwimu ambazo bidhaa zinauzwa sana na kuongeza soko kwa wingi zaidi na itamsaidia mfanyabiashara kufanya maamuzi sahihi kwaajili ya kujikwamua kiuchumi.
Vilevile, TanTrade inatoa fursa za masoko, mabanda ya maonyesho na usafirishaji wa bidhaa kwenda nchi mbalimbali ambapo fursa hizi zitachangia katika kuongeza uchumi binafsi na nchi kwa ujumla. Kadhalika, kutambua takwimu za bidhaa zinazouzwa na nchi mbalimbali kama vile korosho, kahawa, pamba na parachichi.
Pia, kuhusu suala la nishati, TanTrade imeweza kushirikiana na Kenya katika usambazaji wa nishati ya kisasa na iliyo salama na itaendelea kujumuisha nchi mbalimbali ilikukuza soko la nishati vilevile,katika mdahalo amewashauri wajasiliamali kuhusu ufanyaji wa utafiti kabla ya kuleta bidhaa sokoni kwani itasaidia katika kutambua mahitaji ya wateja na kupata njia mbalimbali za kuwa hudumia.
Hivyo, TanTrade ina mchango mkubwa kwa wafanyabiashara na itaendelea kushirikiana nao katika kutangaza bidhaa zao ili kukuza soko binfasi na nchi kwa ujumla