Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania

TanTrade Fostering Business

TANTRADE YASHIRIKI MKUTANO WA MAANDALIZI YA EXPO 2023 DOHA

  • September 11, 2023

10 Septemba, 2023.

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) imeshiriki mkutano wa mwisho wa maandalizi ya Expo 2023 Doha unaofanyika tarehe 10-11 Septemba, 2023, Doha, Qatar.

Mkutano huo umeshirikisha Makamishna wakuu wa Nchi 56 Duniani zinazoshiriki Maonesho ya Kilimo cha Mboga Mboga yanayojulikana kama Doha Horticultural Expo ukiwa ni muendelezo wa matayarisho hayo ambapo Timu ya Expo iliwasilisha hatua za matayarisho kwa makamishna hao ili kurahisisha ushiriki wao katika maonesho yanayotarajiwa kuanza tarehe 2 Octoba, 2023 hadi 28 Machi 2024.
Kwa upande wa Tanzania, mkutano umewakilishwa na Bw.Tahir M.Ahmed na Bi. Mwanaidi K. Chilo kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa Banda la Tanzania, Bi. Latifa M. Khamis, Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade.