Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania

TanTrade Fostering Business

TANTRADE YASHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA KIKAO KAZI CHA WENYEVITI WA BODI NA WATENDAJI WAKUU WA TAASIS ZA UMMA.

  • August 25, 2023

TANTRADE YASHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA KIKAO KAZI CHA WENYEVITI WA BODI NA WATENDAJI WAKUU WA TAASIS ZA UMMA.

Mamlaka ya Maendeleo ya biashara Tanzania (TanTrade) ikiwakilishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Bi. Latifa Khamis imeshiriki katika Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma kilichofanyika Agosti 19, 2023 Jijini Arusha.

Katika Kikao hicho cha Kazi
Mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt.Samia Suluhu Hassan ambaye amewasisitiza Watendaji Wakuu wa Taasisi hiyo kuweka Uzalendo mbele katika kutekeleza majukumu yao na kuwa sehemu ya mabadiliko chanya.
Pia amewataka kuwa tayari kwa mageuzi katika Taasisi za Umma kwa Maendeleo ya Taifa

Pia alieleza kuwa kutakuwa na ushirikiano wa kutosha kutoka Serikalini ili kufikia malengo na kuleta tija kwa Taasisi hiyo.