Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania

TanTrade Fostering Business

TANTRADE YASHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA MAONESHO YA CHAKULA NA KILIMO- AFRIKA (AFRO WORLD AGRI FOOD CONFERENCE AND EXHIBITION)

  • August 13, 2023



...................................................
Na. Norah Thomas-Dar es salaam
10 Agusti,2023.



Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia Taasisi ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) tarehe 10 Agosti hadi 12 Agosti 2023,imeshiriki katika Maonesho ya  kilimo na chakula  Afrika (Afro World Agri Food Conference, exhibition) lililofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee Upanga Dar es salaam,lenye lengo la kuwakutanisha wadau wa Chakula Afrika.


TanTrade ikiwa inatimiza moja kati ya majukumu yake ya kudhibiti Maonesho yote yanayofanyika nchini  ikiwa ni pamoja na Kusimamia  Viwango vya Maonesho ya  Kimataifa yanayofanyika Tanzania hivyo imefanikiwa kuhudhulia kikamilifu katika Maonesho hayo  ili kuhakikisha kuwa yanafuata sheria na Viwango vinavyotakiwa katika kuendesha Maonesho.


Sambamba na  dhima mbalimbali katika Maonesho haya, pia Maonesho yalienda sambamba na Mikutano ya ana kwa ana kwa Wafanyabiashara (B2B) iliyowakutanisha Wafanyabiashara na wawekezaji katika sekta ya Chakula, Viungo, Korosho, Sukari,Maharage , Ngano Pamba, kahawa,  pamoja na Kakao.

Akizungumza katika maonesho  hayo Afisa Biashara kutoka TanTrade Bw.Melkizedeck Salingo amesema kuwa, maonesho hayo   yamekuwa  muhimu sana kwa wadau wote wa Biashara katika Sekta ya Chakula kwani yamewezesha Wadau kujuana kwa ukaribu chini ya Mwamvuli wa Biashara  na kubadilishana mawazo na wadau wengine na kujipatia masoko ya bidhaa zao. 

Aidha  Bw. Salingo ametembelea katika Mabanda mbalimbali ya Wafanyabiashara kutoka India na kuwaelezea majukumu ya TanTrade pamoja na kuwatia  moyo wawekezaji hao kuja kuwekeza na kufanya biashara na nchi ya Tanzania, kwani Tanzania ni mahali sahihi kwa kufanya biashara pamoja na Uwekezaji. 

Naye mmoja kati ya waandaji wa maonesho hayo Bw. Suveer Raj Proheit  ametoa wito kwa wadau wote wa Chakula na Kilimo, kuendelea kujitokeza na kuunga mkono maonesho hayo ili kujihakikishia Masoko ya bidhaa wanazozalisha.

‘’Nawashukuru Wadau wote walioshiriki katika maonesho haya, Hakika wamepata faida kubwa ya kuwepo mahali hapa ikiwemo kujipatia Masoko ya bidhaa wanazozalisha na sambamba na kupata wadau mbalimbali wa kufanya nao kazi, pia napenda Kuchukua fursa hii  kuwakaribisha Wadau wengi zaidi wajitokeze katika  maonesho kwa mwaka ujao’’. Alisema.