Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania

TanTrade Fostering Business

TANTRADE NA KOTRA WAKUBALIANA KUSHIRIKIANA KATIKA BIASHARA NA UWEKEZAJI.

  • August 25, 2023



Mapema leo Tarehe 25 Agosti 2023 TanTrade imefanya kikao kazi na Ujumbe kutoka Taasisi  ya  biashara Korea  Kusini, KOTRA DSM  (Korea Trade-Investment Promotion Agency) chenye lengo la kutaka  ushirikiano wa  kibiashara na Uwekezaji  na kubaini  fursa zinazopatikana katika nchi ya Tanzania na Korea ili kuzitumia ipasavyo kwa lengo la kukuza na kuendeleza  uchumi wa nchi hizo mbili.

Kikao  hicho kimefanyika katika ofisi ya TanTrade barabara ya Kilwa Dar es salaam, pia kimehudhuliwa na Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade Bi. Latifa Khamis, pamoja na Mkurugenzi Mkuu Kamishna wa Biashara kutoka KOTRA Bw. Wohn Jun Young Kwa kushirikiana  na ujumbe kutoka TanTrade na KOTRA.

Katika Kikao hicho Bi. Latifa amesema kwamba, Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia TanTrade ipo tayari kutoa ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji na Taasisi hiyo ili kupanua wigo wa biashara na kuwasaidia Wafanyabiashara  kutoka nchi hizo mbili kuweza kutegemeana kibiashara na kukuza uchumi.

Naye Bw. Whon Jun Young  amesema kuwa KOTRA  imejitolea katika ukuaji thabiti wa  biashara na upanuzi wa soko huku kukiwa na mabadiliko ya dhana katika uchumi wa dunia na mfumo  wa kutambua fursa katika soko la kimataifa hivyo  KOTRA  Inapenda kujenga ushirikiano na Tanzania ili kukuza biashara pamoja na kuchochea mabadiliko aswa kwenye sekta ya viwanda.