TanTrade Yafanya Mkutano na Wanachama wa CTI Kuhamasisha Matumizi ya Nembo ya Taifa – Made in Tanzania
- February 25, 2026
Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade)
imefanya mkutano na wanachama wa Chama cha Wamiliki wa Viwanda Tanzania(CTI)
pamoja na wadau wa sekta ya biashara Tanzania, ikiwa sehemu ya kampeni
endelevu ya kuhamasisha matumizi ya nembo ya Made in Tanzania.
Katika mkutano huo “Mamlaka ya TanTrade imefungua macho ya
wazalishaji kwa kuonyesha kuwa muda umefika wa kuunganisha nguvu kati yao na Serikali katika kuongeza juhudi za
kufikia masoko ya ndani na ya nje ya nchi. Kupitia matumizi ya nembo ya Made in
Tanzania, wazalishaji wanapata fursa ya kutambulika rasmi na serikali, uwezo
wao kuthaminiwa, na bidhaa zao kuunganishwa na masoko ya ndani na nje ya nchi.
Nembo hii ni chombo cha ushindani na heshima ya kitaifa, hususan katika zama
mpya za biashara huria barani Afrika. TanTrade inatoa wito kwa wazalishaji wote
kujisajili sasa ili kunufaika na fursa hizi, kuongeza thamani ya bidhaa zao, na
kujenga imani ya watumiaji kwa bidhaa za Tanzania.”
Wanachama wa CTI na wadau wengine walioshiriki walipata
nafasi ya kutoa maoni na uzoefu wao, wakieleza fursa zinazopatikana kupitia
sekta ya viwanda sambamba na changamoto za gharama za uzalishaji na upatikanaji
wa masoko. Kwa pamoja, walikubaliana kuimarisha kampeni ya Made in Tanzania ili
kuongeza ajira, kukuza uchumi wa taifa, na kujenga imani ya watumiaji kwa
bidhaa za ndani.