TANTRADE YATANGAZA "MADE IN TANZANIA" KATIKA MAONESHO YA 60 YA BIASHARA YA KIMATAIFA (60 FACIM), 2025 MSUMBIJI.
- September 1, 2025
Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) inaendelea kutangaza Bidhaa mbalimbali zinazozalishwa Tanzania kupitia Banda lake la "Made in Tanzania
", katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea nchini Msumbiji. Watembeleaji mbalimbali wamevutiwa na bidhaa hizo ikiwemo Korosho, Kahawa, Chai na Mavazi ya Tanzania.
Aidha, Maonesho haya yanaendelea kufungua fursa za Masoko kati ya Msumbiji na Tanzania na yanataraji kuhitimishwa tarehe 31 Agosti 2025.