BALOZI WA PALESTINA AFANYA MAZUNGUMZO NA MAMLAKA YA MAENDELEO YA BIASHARA TANZANIA (TANTRADE) KUHUSU USHIRIKI WA SABASABA 2026
- April 14, 2026
BALOZI WA PALESTINA AFANYA
MAZUNGUMZO NA MAMLAKA YA MAENDELEO YA BIASHARA TANZANIA (TANTRADE) KUHUSU
USHIRIKI WA SABASABA 2026
———————————
14 Aprili 2026, Dar es Salaam
———————————
14 Aprili 2026, Dar es Salaam
Balozi wa Palestina nchini
Tanzania, Mheshimiwa Salam Abu Sharar, amefanya ziara katika ofisi za Mamlaka
ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) kwa mazungumzo ya maandalizi
ya ushiriki wa taifa lake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya
Dar es Salaam (DITF – Sabasaba 2026).
Katika mazungumzo hayo, Balozi
alieleza kuwa Palestina iko tayari kushiriki kikamilifu katika maonesho hayo
makubwa ya kibiashara, akibainisha kuwa ushiriki huo utakuwa chachu ya
kuitangaza nchi yake kimataifa, kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na kidiplomasia,
pamoja na kuongeza uelewa wa umma kuhusu utamaduni, biashara na fursa zilizopo
nchini Palestina. Aidha, alisisitiza kuwa ushiriki wa Palestina katika DITF
2026 ni sehemu ya mkakati wa taifa lake wa kuimarisha ushirikiano wa kibiashara
na nchi za Afrika Mashariki, hususan Tanzania.
Kwa upande wake, uongozi wa TanTrade
ulimkaribisha rasmi Balozi na kumpatia mwongozo wa taratibu za kupata nafasi ya
maonesho, sambamba na ushauri wa namna bora ya kuandaa na kushiriki kwa ufanisi
katika tukio hilo. Uongozi pia ulisisitiza dhamira ya TanTrade ya kuendelea
kuimarisha ushirikiano wa kimataifa kupitia maonesho ya Sabasaba, ambayo
yamekuwa jukwaa muhimu la kukuza biashara, uwekezaji na diplomasia ya kiuchumi.